You are visitor number

Monday, February 28, 2011

Nitazidi kuongea

nitazidi kuongea

kwa sababu nikiongea

mababu wangu huongea

wale washupavu walionitangulia

zile sauti zilizoshindwa kuongea

wazalendo wangu wanaongea

jamii yangu inaongea

wale niliowajua na wale sikuwajua

wale ambao ninaweza kuwafikiria

lakini cha mhimu

roho yangu inaongea

utu wangu unaongea

ndoto zangu zinaongea

sifa yangu inaongea

mambo mengi sana

kwa hivyo nitaendelea kuongea

nitazidi kuongea

No comments: